March 23, 2014




KIKOSI CHA SIMBA
Simba haitakuwa katika mbio za kuwania ubingwa, lakini unaweza kusema hata nafasi ya pili pia ni nadra.

Kwani leo imepoteza mchezo wake dhidi ya Coastal Union baada ya kufungwa kwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
BOCCO KAZINI

Wakati Simba wakilazwa na Coastal Union iliyojaa vijana, Azam FC wamezidi kujichimbia kileleni baada ya kuifunga JKT Oljoro kwa bao 1-0.
John Bocco ‘Adebayor’ ndiye aliyefunga bao hilo muhimu kwa Azam FC ambayo sasa imefikisha pointi 47, mechi hiyo ilipigwa kwenye Uwanja wa  Azam Complex jijini Dar.
Simba wanabaki na pointi 36 baada ya kupoteza mchezo huo wa Coastal Union licha ya kuwa nyumbani.
Nafasi wanayoweza kuijutia ni ile katika dakika ya 90 aliyoipata Ramadhani Singano ‘Messi’ akiwa amebaki na kipa wa Coastal lakini kashindwa kuusukuma mpira wavuni.
Kupitia Chanongo, Amissi Tambwe na Jonas Mkude, Simba ilipoteza nafasi zaidi ya sita za wazi za kufunga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic