March 23, 2014




Kocha Mkuu we JKT Ruvu, Fred Felix Minziro amesema pamoja na kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mbeya City, jana, bado wana nafasi ya kupambana na kubaki Ligi Kuu Bara.

Minziro ameiambia SALEHJEMBE kwamba kikosi chake bado kina nafasi ya kufanya vizuri na kubaki katika ligi hiyo lakini lazima wajitume.
“Unajua kwenye mpira ukifanya makosa, halafu ukakutana na mtu makini basi ni lazima akuadhibu.
“Mabeki wetu hawakuwa makini ndiyo maana sasa tunajutia lakini pointi tatu dhidi ya Mbeya City zilikuwa muhimu sana.
“Lakini nina imani tutajirekebisha mechi zijazo na kufanya vizuri, tukijituma na kuwa makini, bado tuna nafasi,” alisema inziro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic