March 26, 2014





Mambo yako hivi, mshambuliaji wa Simba raia wa Burundi, Amissi Tambwe, ni bora zaidi ya yule wa Yanga, Emmanuel Okwi, ambaye alijiunga na timu hiyo hivi karibuni akitokea kwenye kikosi cha Villa ya Uganda.

Ubora huo wa Tambwe unatokana na mchezaji huyo kumfunika vibaya Okwi ndani dakika 540 ambazo kila mmoja amezitumia uwanjani hivi karibuni akiitumikia klabu yake kwenye michuano ya ligi kuu na ile ya kimataifa ambayo Yanga ilishiriki.

Tangu mwezi huu uanze Tambwe ameitumikia Simba dhidi ya Mgambo JKT, Prisons, Ruvu Shooting, JKT Ruvu, Mbeya City na Coastal Union, wakati Okwi aliongoza Yanga dhidi ya Ruvu Shooting, Al Ahly, Mtibwa Sugar, Azam na Rhino Rangers.

Championi Jumatano limebaini hilo baada ya kuwafuatilia wachezaji hao katika mechi hizo sita ambazo wamezitumikia klabu zao hizo ndani ya mwezi huu.
Katika uchunguzi huo, ilibainika kuwa Tambwe ndiye aliyefanya vizuri zaidi ya Okwi kwani ndani ya dakika hizo 540 alizoitumikia Simba katika mechi hizo za ligi kuu amefanikiwa kufunga mabao manne.
Kwa upande wake Okwi yeye amezifumania nyavu mara moja katika dakika hizo 540 alizoitumikia Yanga mpaka sasa tangu alipojiunga na klabu hiyo akitokea SC Villa ya Uganda.

Tambwe alifunga mabao hayo katika mechi za ligi kuu dhidi ya JKT Ruvu, Ruvu Shooting na Mbeya City wakati Okwi bao lake hilo alilifunga katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting.
Hata hivyo, Okwi alipoulizwa kuwa ni kwa nini ametumia muda mwingi uwanjani huku akiwa amezifumania nyavu mara moja alisema:  “Wachezaji wengi wananikamia sana hivyo inanibidi nichukue jukumu la kuwatengenezea nafasi za kufunga wachezaji wanzangu na siyo kwamba nimeshuka kiuchezaji, kiwango changu kipo juu ila wananikamia sana,” alisema Tambwe.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic