March 26, 2014

BOUZIANI AKIZUNGUMZA JAMBO WAKATI WA UTAMBULISHO WA SMART MBELE YA WAANDISHI WA HABARI.


Mtandao mpya wa simu wa Smart umepanga kuwajali wanamichezo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Smart, Abdellatif Bouziani, amesema watashirikiana na wanamichezo mbalimbali kadiri siku zitakavyokuwa zinasonga mbele.

Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam, Bouziani alisema mtandao wao utafanya mambo kadhaa ya kijamii na mojawapo ni michezo.

“Kwa sasa tuko katika nchi tatu za Afrika Mashariki, Uganda, Burundi na sasa Tanzania. Tunajua namna michezo inavyopendwa.

“Hivyo tutafanya chini juu kuhakikishia ushirikiano wetu na wanamichezo unakua,” alisema.
Kuhusiana na ushindani,  Bouziani alisema ubora wa mtandao na unafuu ndiyo utakaowavutia wengi.
“Lakini huduma zetu ni nzuri, usione tumeingia sasa Tanzania ukadhani ni wageni katika huduma za simu. Tuko sehemu mbalimbali duniani hivyo tuna uzoefu na ushindani tunauweza,” alisema akionyesha kujiamini.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic