March 15, 2014


NDUMBARO AKIWA MAKAO MAKUU YA FIFA JIJINI ZURICH, USWISS

Simba imetangaza rasmi kuwa uchaguzi wake mkuu utafanyika Mei 4, mwaka huu.
Tarehe hiyo ya uchaguzi imetangazwa rasmi mara tu baada ya kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo kukutana.

Akizungumza leo jijini Dar, Ofisa Habari wa klabu ya Simba, Asha Muhaji amesema Mwanasheria maarufu nchini, Dokta Damas Daniel Ndumbaro ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa kati hiyo ya uchaguzi.
Makamu wake anakuwa, Salum Madenge na Katibu ni Issa Batenga na msaidizi wake ni Khalid Kamguna.

Muhaji aliwataja wajumbe kuwa ni katibu mkuu wa zamani wa Simba, Kassim Dewji, Juma Simba na katibu mkuu wa zamani wa DRFA, Amin Bakhresa.


Kuhusiana na mkutano wake wa kesho, Muhaji alisisitiza Simba itafanya mkutano huo kwa ajenda ileile, moja ya marekebisho katiba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic