April 27, 2014





Kocha Mkuu wa Kenya, Adel Amrouche ametua nchini akiongozana na Mkurugenzi wa Ufundi wa Kenya, Jacob ‘Ghost’ Mulee ili kuipa nguvu timu yao ya vijana.

Amrouche raia wa Ubelgiji amesema kikosi chao cha timu ya taifa ya vijana kina nafasi leo dhidi ya wenyeji Tanzania, Ngorongoro.
Timu hizo za Tanzania na Kenya chini ya miaka 20, leo kwenye Uwanja wa Taifa jijibni Dar zitacheza mechi yao ya pili kuwania kucheza Kombe la Mataifa Afrika kwa vijana. Katika mechi ya kwanza mjini Machakos, Kenya, timu hizo zilitoka sare ya bila bao.
Akizungumza mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam, Amrouche alisema wanaheshimu uwezo wa Tanzania, ila wanachotaka kufuzu.
“Najua kocha wa timu yetu anajua la kufanya, tuko hapa kumuunga mkono na kusaidia ushauri ni kipi cha kufanya. Niko na Mulee hapa na tunaamini Kenya itafuzu,” alisema kocha huyo bora wa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Amrouche ambaye amefikia kwenye hoteli ya Sapphire pamoja na kikosi hicho ambacho kipo nchini siku tatu zilizopita, awali alikuwa Kocha Mkuu wa Burundi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic