April 20, 2014





Coastal Union  ambayo imemaliza Ligi Kuu Bara kwa kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Kagera Sugar, wanachama wake wametoa kali.
 
Wanachama ambao wanaishi mkoani Tanga walitoa ujumbe kwa uongozi wao wakionyesha kupinga mambo kadhaa yanayoonekana kutokwenda sawa.

Lakini kilichoonyesha kweli mambo hayo hayako vizuri ni wachezaji kwenda kuwaunga mkono wanachama hao mara baada ya mechi hiyo kwisha.
Licha ya kuwa wamefungwa, lakini Coastal Union walikwenda kuwapongeza wanachama wao kwa kuwaunga mkono na ujumbe mzuri kwa viongozi.
Uongozi wa Coastal Union, umekuwa ukishutumiwa kukataa kutoa kadi mpya za wachama, huku Kassim El Siagi ambaye ni katibu mkuu akielezwa kuwa chanzo.
Siagi amekuwa akisisitiza kwamba lazima kabla ya kuwakubali wanachama wapya, basi wawahakiki kwanza kwa kuwajadili.
Lakini katiba ya Coastal Union haina kipengele hicho, hali inayoashiria ni uoga wa Siagi na wenzake wanaoohofia huenda wanachama wapya watatokea watu wakaojitokeza kuwania nafasi zao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic