May 4, 2014




KILA zama zina mfalme wake, hiki ndiyo kipindi ambacho karibu kila mtu anayevutia na kocha kijana anayeonyesha uwezo mkubwa analazimika  ku muangalia Diego Pablo Simeone.

Hakuna ubishi ndiye kocha bora na mwenye uwezo wa juu katika wale wanaochipukia katika kipindi hiki kutokana na mafanikio makubwa yanaonekana akiwa na Altetico Madrid.
Tokea aanze kuifundisha timu hiyo mwaka 2011, amekuwa na mafanikio makubwa sana kwa kuwa ameiwezesha kubeba makombe matatu makubwa na maarufu duniani kote, moja likiwa ni lile la Copa de Rey lakini kabla alichukua mawili ya kimataifa ya Europa na Uefa Super Cup.

Hicho kinaweza kuwa ndiyo kigezo cha kwanza ambacho ni uwezo wa kubeba zawadi lakini kigezo cha sasa ni kufanikiwa kufika Ligi ya Mabingwa kwa kishindo akiwapindua makocha na timu bora tena si kwa kubahatisha.
Robo fainali aliibwaga Barcelona yenye nyota kibao, ikaonekana huenda kwa kuwa ni timu ya Hispania wameizoea, kaonyesha sivyo kwani nusu fainali na Chelsea, mechi ya kwanza jijini Madrid ikawa suluhu, waliporudiana London, akampa Jose Mourinho kichapo cha mabao 3-1 na kuifuata Real Madrid fainali.
Sasa Atletico Madrid inapewa nafasi ya kubeba kombe kwa kuwa inakutana na Real Madrid, si timu ya kuihofia sana badala yake watapambana nayo kama mpinzani, mtani na hasimu.
Ile sifa ya kocha kijana, mwenye uwezo mkubwa na mipango ya kutosha aliyokuwa nayo Mourinho, hakuna ubishi imehamia kwa Simeone. Lakini itakamilika kama atatwaa Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya huko Lisbon, Ureno, Mei 21.
 Kuna mambo wanafanana kama vile kufundisha katika nchi zaidi ya moja baada ya kutoka kwao, Mourinho baada ya Ureno amekwenda England, Italia na Hispania na Simeone alipoondoka kwao Argentina amefundisha nchini Italia na Hispania. Pia wamekuwa hawakai na timu muda mrefu kama Alex Ferguson na Arsene Wenger.
Lakini Simeone ana kitu cha ziada kwa kuwa amecheza soka katika ‘levo’ za juu. Pia amewahi kuchukua ubingwa wa La Liga pia Copa del Rey akiwa na Atletico Madrid kama mchezaji, amechukua makombe kadhaa akiwa kwao Argentina na Italia ‘Serie A’. Pia amecheza Kombe la Dunia akiwa na timu yake ya taifa ya Argentina.
Kwa ujumla amechukua makombe 12 yanayotambulika akicheza soka katika ligi za nchi za Argentina, Italia na Hispania, wakati Mourinho hajawahi kubeba kombe hata moja akiwa mchezaji.


TAKWIMU:
Akiwa mchezaji:







































NCHINI               MECHI      MABAO
Argentina          113       17                                                                           
Italia                   202        32                                                                          
Hispania 198        35                                                                          
 JUMLA     513                84         

Akiwa kocha:
Timu alizofundisha:
Racing         2006-06
Estudiantes  2006-07
River Plate    2007-08
San Lorenzo  2009-10
Catania    2011-11

               MECHI    SHINDA  SARE  POTEZA  WASTANI
             348                 19            72           86            54.60%

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic