June 29, 2014



Uchaguzi mkuu wa viongozi wa klabu ya Simba umeanza rasmi sasa hivi.
Uchaguzi huo unafanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Tayari wanachama hao wameanza kupiga kura kuchagua viongozi wao wapya watakaoiongoza Simba kwa miaka minne ijayo.
Nafasi tatu za rais, makamu wa rais, wajumbe wa kamati ya utendaji moja ikiwa ni maalum kwa kinamama, ndiyo zinazogombewa leo.
Mgombea Evans Aveva anapewa nafasi ya kuwa rais mpya wa Simba, lakini Andrew Tupa pia anaweza kutoa upinzani, si wa kumdharau.
Upinzani mkali unaonekana upo kwenye nafasi ya makamu wa rais inayowaniwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, Swed Nkwabi na Geofrey Nyange ‘Kaburu’.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic