ASILIA yake ni
Afrika katika nchi ya Senegal, lakini amekuwa akiichezea timu ya taifa ya
Ufaransa ambayo ameicheza mechi 61 kwa miaka 10, sasa.
Ingawa amekuwa
akitoka na kurejea, Evra ni kati ya wachezaji wachache ambao wameweza kudumu
katika kikosi cha timu ya taifa kwa miaka 10.
Mara ya mwisho
aliichezea Ufaransa kwenye Kombe la Dunia, wiki chache zilizopita nchini Brazil
na kufanikiwa kuvuka hadi hatua ya robo fainali ambapo timu yake iling’olewa na
Ujerumani ambao ndiyo walitwaa ubingwa wa michuano hiyo.
Ukirudi upande
wa klabu, Evra amekichezea kikosi cha Manchester United tokea mwaka 2006, kabla
ya kuamua kufunga safari na kwenda Juventus akiamini wakati umefika hasa baada
ya United kumsajili Luke Shaw.
Shaw lazima
acheze, umri wa miaka 33, unatosha kwake, miaka nane ya kuichezea Man United
inatosha, amehamia Juventus ambayo si timu lelemama pia, hii inaonyesha yuko
fiti kuendeleza soka la ushindani.
Juventus
ambayo rasmi imemtwaa Julai 21, mwaka huu kwa mkataba wa miaka miwili na ada ya
pauni milioni 1.2 ambayo itafikia milioni 1.5 kama itafanikiwa kuingia kwenye
Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, imepata mtu.
Pamoja na
kwamba umri umekwenda, lakini rekodi zake Manchester United, zinaonyesha ni
kati ya mabeki bora, kati ya wachezaji wa kiwango cha juu ambao United imewahi
kuwa nao.
Ilikuwa ni
nadra kwake kuumia, ndiye kati ya wachezaji watano wa juu ambao Kocha Alex
Ferguson, hakuwahi kufikiria kuwabadilisha wakati kikosi chake kinacheza.
Pia ndiyo
mmoja wa wachezaji wachache wa Manchester United, ambao walikuwa fiti kwa
asilimia mia katika mechi zote 38 za ligi katika misimu hadi mitatu.
Ameacha rekodi
nyingi ambazo zinaweza kuwasaidia wachezaji wengi, wakiwemo wale wanaocheza
namba tatu kama yeye, lakini hata wale wanaocheza namba nyingine.
Moja ya sifa
zake ni kutokuwa na ‘mambo mengi’ kama vile starehe za klabu, wanawake wengi,
sigara na kutopumzika.
Akiwa Monaco,
licha ya kuwa na miaka 24, lakini wachezaji wenzake walimbandika jina la ‘Babu’,
maana hakuwa akiongozana nao klabu wala sehemu nyingine za starehe na
alipumzika mwishoni mwa msimu.
Hicho ndiyo
kilikuwa chanzo cha yeye kuanza kufanikiwa na kufikia kuwa mmoja wa mabeki bora
zaidi wa kushoto duniani na ana uhakika wa kuendelea kutamba akiwa Juventus.
Anaweza kuwa
na mambo mengi sana ambayo yatawasaidia wachezaji hapa nyumbani na duniani kote
kama watataka kujifunza kupitia yeye.
Si rahisi
kutaja kila kitu, lakini hizi tano zinaweza kudhihirisha ubora aliokuwa nao.
1. Akiwa na
Man United
Alicheza mechi
273 za Premier.
Akashinda 186.
Sare 43.
Alipoteza 44.
2. Msimu uliopita, Evra alicheza mechi
10 ambazo United walipoteza msimu uliopita na ndiyo nyingi zaidi kuitumikia
klabu hiyo kwa msimu na ikapoteza.
Mfano kwa
msimu wa 2011-12 na 2012-13, yote miwili, Man United, ilipoteza mechi 10.
3. Evra ndiye
alikuwa mchezaji aliyelala na kuokoa mipira mingi kuliko mwingine msimu
uliopita. Alifanikiwa kuokoa hatari 54 kwa njia ya ‘takolin’.
4. Hadi
anaondoka England, ndiye alikuwa mchezaji aliyepiga mipira mingi ya vichwa
akiwa katika nafasi ya pili kutokana na mipira 185. Anayeongoza ni Nemanja
Vidic aliyepiga 199, ambaye amehamia Inter Milan.
5. Ametwaa
makombe & ngao 14:
Makombe 5 ya
Premier
Matajii 5 ya
Ngao ya Hisani
Makombe 3,
Kombe la Ligi
Kombe moja
Ligi ya Mabingwa Ulaya.
0 COMMENTS:
Post a Comment