September 30, 2014

DK NDUMBARO (KUSHOTO) WAKATI AKIWA MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI YA SIMBA.

Klabu 14 za Ligi Kuu Tanzania Bara, sasa zitamtumia mwanasheria maarufu nchini, Dk Damas Daniel Ndumbaro kuwatetea kuhusiana na suala la TFF kukata fedha zao kutoka kwa wadhamini.

TFF imekaa na kujadili, halafu ikakubaliana kuwa fedha za wadhamini kutoka Azam TV na Vodacom, asilia tano zikatwe kutoka kwa kila mdhamini, halafu ziingie TFF kusaidia soka.
Jambo hilo la kwanza la kushangaza katika mchezo wa soka nchini na duniani kote, liliandikwa kwa mara ya kwanza na SALEHJEMBE.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Dk Ndumbaro amethibitisha hilo amesema tayari klabu zimeweka wazi kuhusiana na msimamo wao.
“Klabu zote 14 zinapinga kwa nguvu uamuzi huo wa TFF kutaka kuzikata fedha zao za udhamini wa Azam TV na Vodacom.
“Kuhusiana na mgawo, kila kiko wazi kwamba kila upande unapata kiasi gani.
“Kwa pamoja klabu zina ushauri, kwamba kama kuna fedha inahitajika, basi TFF inaweza kuchukua mgawo wake na kuutumia na si fedha za klabu ambazo zina majukumu mengi ikiwemo kuweka kambi, mishahara na uendeshaji wa timu ili ligi iendelee,” alisema Dk Ndumbaro.

Uamuzi huo wa TFF umeonyesha kuwashangaza wadau wengi hasa kuhusiana na kutaka kuchukua hadi fedha za wadhamini wa klabu. Bodi ya Ligi Tanzania, bado haijatoa uamuzi wake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic