September 28, 2014

 
VITA CLUB
Wakongwe wa DR Congo, Vita Club imefanikiwa kukata tiketi ya kucheza fainali  ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kushinda kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia.

Maana yake Wakongo hao wamefuzu kwa jumla ya mabao 4-2 kutokana na ushindi wa 2-1 katika mechi ya kwanza mjini Kinshasa na sasa wanawasubiri TP Mazembe.
TP Mazembe inacheza leo dhidi ya Entente Setif ya Algeria.
Mazembe inayoongozwa na Mbwana Samatta kwenye safu ya ushambuliaji itakuwa nyumba Lubumbashi.

Vita walikuwa mabingwa wa kombe hilo mwaka 1973 lakini mwaka 1981, wakafanikiwa kuingia fainali.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic