September 28, 2014

CHIPPO

Kocha Mkuu wa Coastal Union, Yusuf Chippo ameendelea kulia kwamba ‘wamenyongwa’ mjini Mbeya.
Chippo raia wa Kenya amesema walifanya kila linalowezekana, lakini mwisho wakapewa penalti ya mizengwe.

“Unajua kama tungekuwa tumefungwa tu, sina sababu ya kulalamika kwa kuwa ndiyo mpira wenyewe.
“Ambacho ningefanya ni kujipanga na kuangalia mechi inayofuata. Lakini tulichofanyiwa si kitu kizuri.
“Wenyeji waliona mambo hayakuwa mazuri na huenda wasingepata penalti ile na kutangulia, basi tungewaangusha, si kitu kizuri kuwa na matokeo ya kuipendelea timu fulani,” alisema Chippo.

Coastal Union imefungwa mechi hiyo kwa bao 1-0 ikiwa ni mechi yake ya pili baada ya kuanza kwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Polisi Moro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic