October 29, 2014


Baba mzazi wa mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete amesema mwanaye sasa amewanyamazisha waliokuwa wakiamini hana lolote.

John Tegete ambaye ni Kocha Mkuu wa Toto African inashiriki daraja la kwanza amesema mwanaye ana uwezo mkubwa wa kufunga na itakuwa vema akipewa nafasi.
Tegete Jr aliifungia Yanga mabao mawili ilipoitandika Stand United mabao 3-0, Jumamosi iliyopita mjini Shinyanga na kuifanya ipande juu katika msimamo wa ligi hiyo kwa kufikisha pointi kumi.
Nyota huyo ambaye alijiunga na Yanga akitokea Shule ya Sekondari Makongo, hivi sasa ndiye anayeongoza kwa kuzifumania nyavu klabuni hapo pamoja na kwamba amecheza dakika 20 tu.
 Tegete Sr alisema kuwa mwanaye huyo amewaziba midomo wale wote waliokuwa wakimchukia na kumfanya akose nafasi katika kikosi cha kwanza cha Yanga licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuzifumania nyavu kuliko mchezaji mwingine klabuni hapo kwa hivi sasa.
Alisema kitendo cha mwanaye huyo kuwa benchi muda mwingi bila ya kucheza kilikuwa kikimuumiza sana na alikuwa akiwapigia kelele mara kwa mara viongozi wa Yanga juu ya jambo hilo, lakini waliziba masikio kwa sababu tu ya chuki binafsi.
“Siku zote nilikuwa nikimwombea mazuri mwanangu juu ya wale wanaomchukia kwa kila nilipokuwa nikiwauliza kwa nini hachezi, waliniambia kuwa hachezi kwa sababu anapokuwa uwanjani hufanya mzaha, jambo ambalo si kweli kabisa, Tegete hayupo hivyo ila yeye ni mtu wa watu na hupenda kucheka na kutaniana na kila mtu.
“Hata hivyo, pamoja na yote hayo, namshukuru Mungu, mwanangu ameonyesha kuwa yeye ni bora zaidi katika kikosi cha Yanga hata kama wanamchukia lakini atabakia kuwa bora,” alisema Mzee Tegete ambaye pia ni kocha mkuu wa timu ya Toto African ya jijini Mwanza.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic