October 1, 2014

MWENYEKITI MTENDAJI WA PAP/IPTL, HARBINDER SINGH SETHI (KUSHOTO) AKIKABIDHI MFANO WA HUNDI WA SH MILIONI 20 KWA MWENYEKITI WA TASWA, JUMA PINTO. WENGINE WANAOSHUHUDIA NI VIONGOZI WENGINE WA TASWA, KATIBU MKUU AMIR MHANDO NA EGBERT MKOKO.

Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI  ya kufua umeme ya Pan African Power Solution inayoimiliki kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imedhamini tuzo ya Mwanamichezo bora wa  chama cha Waandishi wa Habari nchini (Taswa).


Kampuni hiyo leo ilikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 20, kwa uongozi wa chama hicho ikiwa ni njia mojawapo ya kusaidia michezo hapa nchini.

Taswa ambayo imekuwa ikiandaa tuzo ya mwanamichezo Bora, inahitaji kiasi cha shilingi milioni 120, ili kufanikisha utoaji wa tuzo hiyo baadaye mwaka huu.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya hundi hiyo, Mwenyekiti wa IPTL, Harbinder Sigh Sethi, alisema wametoa msaada huo ili kuchangia tasnia ya michezo hapa nchini.


“ Siyo kwamba IPTL tuna fedha nyingi sana, au ni matajiri sana, bali tunafanya hivi ili kuchangia michezo hapa nchini.

“Tunayaomba na makampuni mengine yajitokeze kwa ajili ya kuwasaidia Taswa, kwa kuwa jambo wanalofanya ni zuri sana hapa nchini Tanzania. Huu kwetu ni mchango kidogo, lakini ni vizuri na makampuni mengine yakajitokeza kusaidia,” alisema Sethi ambaye aliwahi kushiriki mbio za magari za ubingwa wa Afrika.

Naye mwenyekiti wa Taswa, Juma Pinto, ambaye alipokea hundi hiyo alisema wanaishukuru IPTL kwa msaada huo kwani ni jambo jema kwa kampuni kama hiyo kujitokeza kusaidia michezo hapa nchini.

“Bado tunahitaji kubwa sana. Tunatakiwa kupata milioni 120 ili kufanikisha tuzo za mwaka huu. Ni vizuri tukiwashukuru sana IPTL kwa msaada wao, tunajua kuwa utatufikisha sehemu fulani.

“Tunaomba na makampuni mengine yajitokeze ili kutusaidia kutoa tuzo ya mwaka huu kwa mafanikio makubwa,” alisema Pinto.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic