October 5, 2014

SHABIKI MBEYA CITY, AKIONYESHA ALIVYOJERUHIWA.

Uongozi wa Mbeya City umetoa tamko la kulaani kupigwa kwa mashabiki wao kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting iliyopigwa kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani, jana.

Mechi hiyo ilimalizika kwa suluhu na kuwa sare ya pili ya Mbeya City dhidi ya timu za jeshi. Mechi ya kwanza mjini Mbeya iliyoka sare na JKT Ruvu.
Uongozi huo kupitia Ofisa Habari wake, Dismas Ten umesema kuwa sehemu hiyo si salama. Soma tamko lao.
“Inasikitisha sana, wanajeshi jana walianza kuwapiga mashabiki wa Mbeya City FC, kwa  sababu  walikuwa wakizunguka uwanjani kushangilia.
“Tatizo lilianza pale walipokwenda kwenye lango la Mbeya City na kipa wetu David Buruhani muda wote  alikuwa akibughuziwa na kundi la watu wanaoaminika ni askari lakini walikuwa wamevaa kiraia.

“Ghafla Wanajeshi wakaja juu na kuanza kuwapiga mashabiki wetu, Uwanja wa Jeshi timu ya Jeshi, kuna haja TFF kuangalia hili.
“Raia wananyanyasika! Uwanja wa Mabatini siyo sehemu salama kwa raia hasa timu yao inapokuwa na matokeo mabovu, uwanjani kunakuwa hakuna ruhsa ya kushangilia timu pinzani.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic