November 2, 2014

MWADUI
Kikosi cha Toto African ya Mwanza, kimeichapa FC Panone katika mechi ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Toto African inayofundishwa na John Tegete, baba mzazi wa mshambuliaji Jerry Tegete wa Yanga, imeibuka baada ya kupoteza mechi iliyopita lakini iko kwenye listi ya timu zilizoshinda mechi tatu.
Wakati Toto inashinda, Mwadui FC inayofundishwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ imeichaoa Rhino Rangers ya Tabora kwao kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.
Kikosi hicho cha Julio kilipata mabao yake kila kipindi na kujiweka vizuri kwenye vita ya kurejea Ligi Kuu Bara.

Ashanti nayo ilichezea kipigo kutoka kwa Tesema wakati Lipuli nayo iliibuka kwa kupata ushindi baada ya kuwa ikiambulia sare na vipigo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic