November 26, 2014


Siku mbili tu baada ya kujiunga na kuanza mazoezi na kikosi cha Azam FC, aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Simba, Amri Kiemba, amesema amejiunga na timu hiyo kwa ajili ya kucheza mashindano ya kimataifa.


Azam FC itaiwakilisha Tanzania Bara katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayoanza kutimua vumbi mwakani baada ya kupata tiketi hiyo kutokana na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita.

Kiemba amesema kuwa tangu aliposhiriki mashindano hayo miaka mitatu iliyopita akiwa na Simba na kufanikiwa kufanya vizuri, alikuwa na hamu kubwa ya kuendelea kufanya hivyo lakini ndoto hizo zilikwama.

Alisema  hali hiyo ilikuwa ikimkosesha amani, lakini baada ya kutua Azam FC, amepata matumaini mapya, hivyo Mungu akimjalia uzima atatimiza ndoto yake.

“Lakini pia nitakuwa nafanikiwa kuandika rekodi ya kuwa miongoni mwa wachezaji wachache wa hapa nchini waliowahi kushiriki mashindano hayo wakiwa na klabu tatu tofauti.

“Kwa mara ya kwanza nilishiriki mashindano hayo nikiwa na Klabu ya Yanga, baadaye Simba na sasa Mungu akipenda nitashiriki nikiwa na Azam, hakika nina furaha sana na ninaamini kuwa nitafanya vizuri,” alisema Kiemba.

Kiemba amejiunga na Azam FC kwa mkopo wa miezi sita ikiwa ni baada ya uongozi wa Simba kumsimamisha pamoja na wachezaji wenzake, Haruna Chanongo na Shabani Kisiga kwa madai ya utovu wa nidhamu.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic