November 26, 2014


Na Saleh Ally
MMOJA wa makocha ambao hawatapotea katika historia ya Klabu ya Simba kwa kipindi kirefu ni Milovan Cirkovic.


Milovan, raia wa Serbia, amekuwa mmoja wa makocha waliopendwa zaidi katika klabu ya Simba na amewahi kuifundisha kwa vipindi viwili tofauti.

Kocha huyo mtaratibu katika mazungumzo, ndiye aliiongoza Simba katika msimu mmoja kuifunga Yanga mabao 5-0, pia kubeba ubingwa wa Tanzania Bara.

Milovan aliiongoza Simba kuwa na kikosi kinachocheza soka la uhakika na hata mabingwa wa sasa wa Afrika, Setif ya Algeria, walitua jijini Dar es Salaam na kulambwa mabao 3-1 na baadaye kutolewa kabisa kwenye michuano hiyo.

Hakuna ubishi, kikosi cha Simba wakati huo kilikuwa moja ya vikosi bora vilivyowahi kutokea katika klabu hiyo.

Mei 6, 2012, Simba ilitoa kipigo hicho cha mabao 5-0 kwa Yanga katika mechi ya kumalizia Ligi Kuu Bara. Hiyo ni sehemu ya kumbukumbu ya kocha huyo ambaye sasa ni Kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya Myanmar.

Mechi hiyo ni gumzo zaidi kwa mashabiki wa Yanga na Simba. Haijasahaulika na huenda ikachukua muda kutoka midomoni na masikioni mwa mashabiki wa soka.

Wakati Milovan anaondoka nchini, Simba ikiwa chini ya Ismail Aden Rage, aliwaambia mashabiki wa soka nchini kwamba ushindi kama huo kwa Simba au Yanga, utatokea baada ya miaka mingine mingi au utatokea si kwa kutarajia, hivyo Yanga hawana sababu ya kupambana kutaka kulipa katika mechi wanayocheza.

Milovan anaendelea na kazi yake vizuri katika nchi hiyo ndogo ya Bara la Asia na sasa yuko nchini Singapore ambako kuna michuano ya Suzuki Cup.

Michuano hiyo inashirikisha timu nane zilizo katika makundi mawili na inachezwa katika nchi mbili za Singapore na Vietnam.

Akihojiwa na SALEHJEMBE kutoka Singapore, Milovan anasema ameendelea kuwa mpenzi mkubwa wa Simba na kamwe hajawahi kuusahau ushindi wa mabao matano dhidi ya Yanga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic