November 21, 2014


Katika kuhakikisha inafanya vema kwenye Ligi Kuu Bara, Ndanda FC ya Mtwara imeamua kusajili wachezaji kutoka Burundi na katika timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.


Ndanda inayoshika nafasi ya pili kutoka mkiani katika msimamo wa ligi kuu, tayari imeshaingia mkataba na kiungo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Masoud Ally Mohamed ‘Chille’ ambaye kwa sasa anaichezea Zanzibar Heroes.

Klabu hiyo imeanza mazungumzo na mashambuliaji, Indeshyme Dumu raia wa Burundi ambaye alikuwa anacheza soka la kulipwa nchini Djibouti.

Katibu wa Ndanda, Selemani Kachele ameliambia Championi Ijumaa kuwa, nia yao ni kusajili wachezaji sita wakati huu wa dirisha dogo.

“Lengo letu ni kuhakikisha tunaiboresha timu yetu kabla ya ligi kuanza kwa kuhakikisha tunasajili wachezaji wenye kiwango,” alisema Kachele. KATIKA kuhakikisha inafanya vema kwenye Ligi Kuu Bara, Ndanda FC ya Mtwara imeamua kusajili wachezaji kutoka Burundi na katika timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes.

Ndanda inayoshika nafasi ya pili kutoka mkiani katika msimamo wa ligi kuu, tayari imeshaingia mkataba na kiungo wa zamani wa Mtibwa Sugar, Masoud Ally Mohamed ‘Chille’ ambaye kwa sasa anaichezea Zanzibar Heroes.

Klabu hiyo imeanza mazungumzo na mashambuliaji, Indeshyme Dumu raia wa Burundi ambaye alikuwa anacheza soka la kulipwa nchini Djibouti.

Katibu wa Ndanda, Selemani Kachele amesema nia yao ni kusajili wachezaji sita wakati huu wa dirisha dogo.


“Lengo letu ni kuhakikisha tunaiboresha timu yetu kabla ya ligi kuanza kwa kuhakikisha tunasajili wachezaji wenye kiwango,” alisema Kachele.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic