December 19, 2014



Kocha Mkuu wa Simba, Mzambia, Patrick Phiri, ametoa yake ya moyoni na kusema kuwa kama kweli Yanga imemtimua kocha wake, Mbrazili, Marcio Maximo basi haikuwa sahihi kwa sababu alikuwa tayari ameshakaa katika mstari.


Kocha huyo aliyewahi kuinoa timu ya taifa ya Zambia 'Chipolopolo', amesema kuwa, kitendo cha klabu kutimua makocha baada ya muda mfupi si kizuri kwa sababu kinaharibu programu za mwalimu husika, ingawa hawezi kuingilia masuala ya Yanga.

“Unajua kila kocha ana vitu vyake anavyovifanya katika timu, sasa ikitokea akatimuliwa kabla hajakamilisha ni tatizo, kwa kuwa atakayekuja ataanza upya.

“Uongozi wa Yanga una kitu umeona unataka kurekebisha na njia mojawapo ni kutokuwa na Maximo, hilo siwezi kuwashambulia kwa sababu wao wanaijua zaidi Yanga.


“Nilikutana naye (Maximo) na tulizungumza baada ya mchezo, Maximo ni rafiki yangu mkubwa tunapokutana nje ya uwanja, ninafikiri huu ni muda mzuri wa kujitafakari, makocha kufukuzwa ni kawaida, ninafikiri analijua hilo,” alisema Phiri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic