January 16, 2015

COUTINHO...

Bosi wa benchi la ufundi la Yanga, Han van Der Pluijm, amembadilishia jina kiungo wake mshambuliaji, Andrey Coutinho na sasa anamuita Romario de Souza Faria.


Romario ni straika wa zamani wa Brazil aliyetamba miaka ya 1990 mpaka 2000, hasa kwenye kikosi cha taifa cha Brazil.
PLUIJM

Kocha huyo raia wa Uholanzi, alianza kusikika akimfananisha Coutinho na Mbrazili mwenzake huyo katika mazoezi ya Yanga yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Boko Veterani uliopo Ununio jijini Dar es Salaam, juzi.

Pluijm alikuwa akimuita Coutinho kwa jina hilo la Romario kila alipokuwa akitaka kutoa maelekezo kwake na kiungo huyo hakusita kuitikia.

Alipoulizwa kocha huyo sababu ya kumuita jina la Romario alifunguka: “Sitamuita jina la Coutinho tena, sasa nitamuita Romario kutokana na aina yake ya uchezaji kufanana na Romario.”


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic