January 16, 2015

MWALALA WAKATI AKIICHEZEA YANGA...

Katika hali ya sintofahamu, Kocha Msaidizi wa Coastal Union, Ben Mwalala, ametimka katika kikosi hicho na kurejea nchini kwao kutokana na kuwepo kwa madai ya masuala ya kimaslahi na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa kocha wa Mgambo msimu uliopita, Mohamed Kampira.


Mwalala alikuwa akisaidiana na Mkenya mwenzie, Yusuf Chipo ambaye naye alibwaga manyanga katika kikosi hicho kwa madai anakabiliwa na matatizo ya kifamilia na kushindwa kurejea nchini.

“Mwalala ameondoka kutokana na masuala ya kimaslahi baada ya kushindwana na klabu, japo mpaka sasa haijaweka wazi suala hilo na hii inakuwa kama ilivyotokea kwa Chipo,” kilisema chanzo.


 Ofisa Habari wa Coastal, Oscar Assenga ambaye amesema: “Mwalala hayupo na sina taarifa zozote, kuhusu Kampira kuonekana kwenye benchi siyo tatizo, ni mmoja wa viongozi wa benchi la ufundi la timu yetu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic