January 17, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amemuweka faragha kiungo wake Andrey Coutinho raia wa Brazil na kufanya naye mazungumza.

Habari za uhakika kutoka Yanga zimeeleza kwamba Pluijm raia wa Uholanzi alikaa na Coutinho na kuzungumza naye mambo kadhaa kuhusiana na timu.

“Kweli kocha alikaa na Coutinho tukiwa Zanzibar na kumtaka acheze soka, ajiamini na ajue kazini pia aachane na maneno ya hisia.

“Unajua awali kulikuwa na taarifa kwa kuwa Mbrazili mwenzake, Marcio Maximo ameondoka basi Pluijm hatampanga,” kilieleza chanzo.

Baadaye juhudi za kumpata Pluijm kuhusiana na suala hilo zilifanikiwa, naye akasema kuzungumza na mchezaji wake ni jambo la kawaida.

“Ninazungumza na Coutinho na wachezaji wengine mara kadhaa. Maneno yanaweza kuwa ya aina nyingi, lakini najua Coutinho ni mchezaji anaijua kazi yake.

“Pia niseme, Coutinho ni mchezaji mzuri. Hivyo ninaweza kumhimiza ajitume au kubadilisha kitu na kukaa naye si jambo geni,” alisema Pluijm.

Maximo alitupiwa virago vyake na nafasi ikachukuliwa na Pluijm ambaye anaonekana kuibadili timu na sasa inacheza kwa kasi kubwa.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic