January 15, 2015

MWAMUZI WA AKIBA AKITIMUA MBIO HUKU MMOJA WA VIONGOZI WA POLISI TABORA AKITAKA KUMKAMATA...
Waamuzi wengine wamepigwa tena na timu inayomilikiwa na Jeshi la Polisi Tanzania!


Mamuzi wa kati na msaidizi wake wameambulia kipigo jana kutoka kwa wachezaji wa Polisi Tabora.
 
MWAMUZI WA KATI NAYE AKIVAMIWA NA WACHEZAJI WA POLISI KABLA YA KUANGUSHIWA KIPIGO...
Kipigo hicho wamekipata kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ikiwa ni siku moja baada ya wachezaji wa Polisi Dodoma kwenye uwanja huo kumtandika mwamuzi.

Wachezaji wa Polisi Tabora waliingia jazba baada ya Toto African kusawazisha bao na kuongeza jingine ndani ya dakika mbili tena dakika ya 90.

Baada ya bao la pili walimvamia mwamuzi wa akiba Agustine Mapalala wa Geita maarufu kama mshika kibendera na kuanza kumshushia kipigo.

Alipoona mambo magumu alianza kutimua mbio na wao wakahamishia hasira zao kwa mwamuzi wa kati Jamada Amada kutoka Kagera.

Hata hivyo, askari waliokuwa uwanjani waliamua kuingilia na kuzuia tukio hilo na mwamuzi alikimbizwa kwenye chumba cha VIP.


Baadaye mwamuzi alirudi chini ya ulinzi mkali na kumaliza mpira huku tayari wachezaji wa Polisi Tabora wakiwa wametoka nje ya uwanja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic