January 15, 2015


Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm ameonyesha kutilia mkazo katika suala la kutengeneza nafasi na kuzutumia.


Katika mazoezi ya leo alitumia zaidi ya nusu saa akiwanoa wachezaji wake hasa walio kwenye safu ya ushambuliaji kama Kpah Sherman, Coutinho, Mrisho Ngassa, Amissi Tambwe, Nizar Khalfan, Jerry Tegete na Simon Msuva.


Pluijm alikuwa akiwanoa washambuliaji wake hao kuhusiaa na suala la kutulia kila wanapotakiwa kuutumbukiza mpira wavuni.

Mholanzi huyo amekuwa akilalama kwamba wanapata nafasi, lakini hazitumiki.


“Ni kati ya mambo niliyotilia mkazo. Tunahitaji mabao na ikiwezekana mengi na mechi ya wikiendi hii itakuwa kipimo kwa tunachofanya sasa,” alisema Pluijm.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic