February 19, 2015

KIKOSI CHA RUVU SHOOTING
Msemaji wa JKT, Masau Bwire amesema mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Azam FC wamepata bahati ya mtende kupata sare.


Azam FC imetoka sare ya bila kufungana dhidi ya Ruvu Shooting katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi, Pwani.
MASAU BWIRE.
Masau amesema kupoteza nafasi nyingi kumechangia wao kuwakosa Azam.

“Tuliwazidi kila kitu, tulikuwa na uhakika wa kuwashinda. Basi tu tulipoteza nafasi wenyewe.
“Kwa kweli Azam FC wanapaswa kushukuru kwa kuwa na bahati hiyo,” alisema.

Kwa upande wa Azam FC, msemaji wao, Jaffar Iddi amesema uwanja mbovu ndiyo ulichangia wao kutoibuka na ushindi.

“Ilikuwa si lahisi kucheza katika kiwango chetu kwa kuwa uwanja wa Mabatini ni mbovu sana na haustahili kabisa kuchezewa.


“Ukiangalia kwa juu, unaweza kudhani ni uwanja mzuri lakini ni mbaya na una mabonde mengi,” alisema Jaffar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic