February 19, 2015

Klabu ya Chelsea imetangaza kuwasimamisha mashabiki wake watatu kuingia kwenye Uwanja wa Stmaford Bridge, London.


Chelsea imewazuia mashabiki hao baada ya kubainika walishiriki katika kitendo cha ubaguzi dhidi ya mtu mmoja mweusi jijini Paris, Ufaransa.

Mashabiki hao walimsukuma mtu huyo wakimzuia kuingia kwenye treni wakati wakiwa wanakwenda kuangalia mechi yao ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya PSG.
Mtu huyo alijaribu kuingia kwenye treni lakini walimsukuma huku wakiimba “Sisi ni wabagusi, sisi ni wabaguzi”.
MTU ALIYEZUIWA KUINGIA KWENYE TRENI NA MASHABIKI HAO AKIWA NJE YA TRENI BAADA YA KUSUKUMWA...

Kitendo hicho kimeonekana kwenye picha ya video na kuwaudhi wadau wengi wa michezo na wamekuwa wakisisitiza wachukuliwe hatua.

Chelsea imetangaza kuwasimamisha kuhudhuria kwenye uwanja wake na uchunguzi unaendelea kufanyika. Iwapo watabainika kushiriki moja kwa moja, basi watakungiwa maisha.


BLOG HII INALAANI VITENDO VYA KIBAGUZI KAMA HIVYO VILIVYOFANYA NA MASHABIKI WA CHELSEA KUWA NI UPUUZI MKUBWA.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic