February 18, 2015


Pamoja na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya BDF XI ya Botswana katika mchezo wa kimataifa wa Kombe la Shirikisho Afrika wikiendi iliyopita, kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mnyarwanda, Haruna Niyonzima, amesema ana hofi na mchezo wa pili.


Yanga inatarajiwa kurudiana na BDF XI Februari 28 nchini Botswana na itatakiwa kuhakikisha inafanya vizuri katika mechi hiyo ili iweze kujikatia tiketi ya kusonga mbele kwenye hatua nyingine ya michuano hiyo.

Niyonzima amesema bado wana kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha wanasonga mbele kwenye mashindano hayo kutokana na ubora wa wapinzani wao.

 “Wito wangu kwa kocha ni kuhakikisha anaufanyia kazi upungufu wote uliojitokeza katika mechi yetu ya kwanza ili usije kutusababishia matatizo tutakaporudiana.

“Mabao mawili siyo mengi sana na hivyo tusipojiandaa vizuri tunaweza tukajikuta tunatupwa nje, tunatakiwa kwenda kwa nia ya kushinda au kupata sare yoyote,” alisema Niyonzima.

Katika mechi dhidi ya BDF jijini Dar es Salaam, Niyonzima alicheza katika kiwango kizuri na kuwa mwiba kwa safu ya kiungo na ile ya ulinzi ya Waswana hao.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic