MPIRA UMEKWISHA
DK 88 baba Ubaya anapewa kadi ya njano kwa madhambi
Dakika za
mwisho Simba wanacheza mpira wa pasi zaidi kuonyesha wameridhika na bao tatu
huku Ruvu nao wakionyesha kukata tamaa.
Dk 81
Simba wanamtoa Tshabalala na nafasi yake inashukuliwa na Issa Rashid ‘Baba
Ubaya’
Dk 75
Maguri anaifungia Simba bao la tatu baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa
baada ya shuti Ndemla aliyewachambua mabeki.
Dk 72, Ruvu wanamtoa Juma Nade na nafasi yake inachukuliwa na Juma NdindiDk 71Singano, akiwa katika nafasi nzuri kabisa, anashindwa kufunga huku kiopa akiwa ameacha wazi sehemu kubwa ya lango.
Dk 69, Simba wanamtoa Okwi na nafasi yake inashukuliwa na Elius Maguri.
GOOOOOOOOO DK 61, Awadhi anawachambua mabeki wa Ruvu na kupiga shuti kali linalomgonga beki na kujaa wavuni.
GOOOOOOOO Dk 60 Ajibu Anafunga vizuri mkwaju wa penalti na kuipa Simba bao.
PENAAAAAAT Dk 58 Awadhi Juma anaagusha katika eneo la 18, mwamuzi anaweka mkwaju wa penalti
DK 55, Tumbo anapata pasi nzuri, nafasi nzuri lakini yeye na lango, nashindwa kufunga.
Kipindi cha pili kinaanza kwa kasi kubwa, Simba kama walivyoanza kipindi cha kwanza. Wanakianza cha pili kwa kasi kubwa wanapeleka mashambulizi mfululizo lakini vilevile wanashindwa kutumia nafasi.
MAPUMZIKO:
Okwi anapiga shuti kali linagonga mwamba na kutoka kurudi uwanjani
Dk 45+3
Dk 44 Okwi analambwa kadi ya njano kwa kushika mpira
Dk 39, Okwi anapi mpira dhaifu wakati unaelekea langoni, mabeki Ruvu wanautoa na kuwa kona
Dk 34, Tumbo anapiga kichwa safi lakini kipa Peter Manyika anadaka kwa ulaini
Dk 29, THIS IS TOO MUCH aisee, Okwi tena akiwa hatua tatu kutoka lango la Ruvu, anapiga kichwa cha kuchumpa kinatoka nje. Eh!
Dk 21 Yayaha Tumbo anakimbia na kupiga shuti kali linalopaa. Hili ndiyo shambulizi la kwanza la Ruvu Shooting langoni mwa Simba.
Dk 18, Ajibu anazuga kama anatoa pasi, lakini mpira unapaa kidogo.
Dk 10,
Simba wanapoteza nafasi tena, safari hii akiwa amebaki na kipa baada ya
mabeki kuaguka.
Dk 6 Simba
wanapoteza nafasi nyingine baada ya kuteleza na kuanguka na kushindwa kufunga
krosi nzuri ya Singano.
Dk 3,
Ajibu anapokea krosi safi ya Kessy na kupiga kichwa kinapaa juu
Dk 2 Okwi
anaingia kwenye lango la Ruvu lakini kipa anajotokeza na kudaka
Dk 1 Simba
wanafanya shambulizi kali lakini mpira unaokolewa na mabeki Ruvu.
0 COMMENTS:
Post a Comment