March 21, 2015


Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal ameamua kuweka wazi mipango yake ya kustaafu kufundisha soka ambapo amesema klabu hiyo ndiyo ya mwisho na baada ya hapo ataachana na kazi ya ukocha.


Van Gaal, 63, amesema hayo muda mfupi kabla ya mechi dhidi ya Liverpool ambayo inatarajiwa kupiga kesho Jumapili kwenye Uwanja wa Anfield.

Kocha huyo raia wa Uholanzi ameweka wazi kuwa nia yake kwanza ni kuhakikisha United ambayo inamiliki Uwanja wa Old Trafford inapata mataji kisha ndiyo atang’atuka.

“Umri umesogea, hii itakuwa kazi yangu ya mwisho, nahitaji kuwa karibu na watoto wangu, wajukuu wangu na mke wangu.

“Wanastahili kuwa karibu yangu, sasa hivi siwezi kuwa karibu nao mfano nilikosa sherehe ya kuzaliwa ya mjukuu wangu, sikupenda,” alisema kocha huyo.

Kuhusu mwelekeo wa timu yake, alisema: “Tunao ubora wa kucheza Ligi ya Mabingwa, kuna maendeleo ya timu kadiri siku zinavyosogea.

“Nahodha wangu, Wayne Rooney ni mwepesi wa kuelewa, sijui kama huwa anazungumza na mkewe kuhusu soka, ninachomaanisha ni kuwa wachezaji wangu wengi ni watu waelewa.

“Mfano mwingine ni Michael Carrick naye ni zaidi ya mchezaji, anajua vitu vingi na anapenda kuzungumza kuhusu mbinu, nafurahi kufanya kazi na wachezaji waelewa.”



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic