April 11, 2015

KASEKE (WA KWANZA KULIA) AKIWA NA KIKOSI CHA MBEYA CITY.
Kama kweli Simba na Yanga zinataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Mbeya City, Deus Kaseke basi zijiandae kuvunja benki na kumlipa daua la shilingi milioni 45 ili ajiunge na moja kati ya timu hizo.


Mkataba wa Kaseke na Mbeya City unafikia tamati mwishoni mwa msimu huu, tayari Simba na Yanga zimeshaonyesha nia ya kumsajili Kaseke lakini zilishindwa kuvunja mkataba wake Desemba, mwaka jana katika dirisha dogo la usajili.

Kwa mujibu wa kanuni, Kaseke anaruhusiwa kufanya mazungumzo na timu yoyote yenye nia ya kumsajili na rafiki wa karibu wa winga huyo, aliliambia Championi Jumamosi kuwa; “Kaseke anataka shilingi milioni 45 ili aweze kusaini Simba au Yanga.

“Pia anataka alipwe mshahara mzuri ambao watakubaliana na kulipiwa nyuma ya kuishi jijini Dar, lakini bado anatoa nafasi kwa timu yake ya Mbeya City kama nayo itakubaliana naye kuhusu usajili mpya.”


Alipotafutwa na gazeti hili, Kaseke alithibitisha kuzungumza na Simba na Yanga na kuongeza; “Soka ndiyo ajira yangu kama kuna timu itakuwa na mimi sina kinyongo lakini kwa sasa natazama mechi  yetu na Yanga ya keshokutwa (kesho).”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic