April 11, 2015


Hali si nzuri kwa mbaya kwa Mtibwa Sugar na Prisons katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, lakini timu hizo zimekomaa na kusema hazitakubali kushuka daraja.


Prisons inashika mkia katika ligi hiyo yenye timu 14 ikiwa na pointi 20 na Mtibwa ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 23, zote zimecheza mechi 20 na zina michezo sita tu.

Kocha wa Mtibwa, Mecky Maxime alisema; “Nitapambana ili tusishuke daraja japokuwa ligi ni ngumu na matokeo mengine yanakatisha tamaa kwani kila mara tunajipanga kupata ushindi lakini mambo yanageuka.”

Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Prisons, Lupyuto Mwanguku alisema kikosi chao kinapambana kupata pointi 18 katika mechi zake sita zilizobaki ili kisishuke daraja.

“Kweli ligi ngumu na tumebakisha mechi sita tu, tunataka tushinde zote ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kubaki katika ligi na hilo linawezekana,” alisema Mwanguku.


Mtibwa, leo Jumamosi inacheza na Azam FC kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, wakati Prisons itacheza na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic