April 11, 2015



Na Saleh Ally
SWALI la kwanza, unawazuia vipi Juventus wasiwe mabingwa wa Italia, maarufu kama Serie A?
Hadi sasa wana pointi 70 wakiwa ndiyo vinara wa msimamo wa Serie A. Wanaowafuatia AS Roma wana pointi 56, tofauti ya pointi 14.

Mechi zilizobaki ni tisa tu, Juventus itacheza nne nyumbani na tano ugenini huku mfumo ukionyesha itakuwa hivi, mechi moja nyumbani, moja ugenini hadi watakapomaliza.

Kama Roma watashinda mechi zao zote tisa zilizobaki watafikisha pointi 83. Maana yake Juve wanatakiwa kushinda mechi tano kati ya tisa wajihakikishie ubingwa maana watakuwa na pointi 85.

Uwezo wa kushinda mechi hizo wanao? Takwimu za mechi sita zilizopita zinawabeba kwa kuwa wameshinda mechi tano na kutoka sare moja.

Timu inayoonekana kuwa na rekodi nzuri zaidi ya Juve kwa mechi sita zilizopita ni Lazio ambayo imeshinda zote, hata hivyo iko katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 55, bado haiwezi kuwa presha kwa Juve.

Takwimu za mechi hizo zilizopita zinaonyesha kuwa Juve tayari imeusogelea kwa mara nyingine ubingwa wa Italia kwa asilimia 90.

Ubora wa kikosi chake unaoongozwa na Carlos Teves ambaye ameshaifungia timu hiyo mabao 17, unaonyesha hawatazuilika na wenyewe ndiyo wamiliki wa Italia katika soka.
 
Ufalme wa Juve unaonekana kuzidi kutanuka na kuimarika zaidi kutokana na wakongwe wengine kupoteza kabisa mwelekeo.
Wakongwe wenzake, yaani AC Milan na Inter Milan ni choka mbaya kabisa, maana wapo katika nafasi ya za nane na tisa katika msimamo huo wa timu 20.

Hadi sasa Juve ndiyo timu yenye safu kiwembe ya ushambuliaji, imefunga mabao 57 na ina ngome ngumu, imefungwa 14 tu huku iliyofungwa mengi zaidi ikiwa ni Cagliari iliyotunguliwa mara 56.

Juve imefunga mabao 36 na 26 yakiwa ni ya ugenini. Imefungwa saba ugenini na saba nyumbani kukamilisha hiyo 14 ambayo ni idadi ndogo zaidi msimu huu.

Kiungo kinachoongozwa na mkongwe Andrea Pirlo na bwa’mdogo Paul Pogba, kinaifanya Juve kuwa timu iliyounganika vema.

Kwa hali inavyokwenda, inaonekana hakuna wa kuizuia Juve kutwaa ubingwa wa 31 wa Serie A. Soka ni mchezo wenye maajabu yake, lakini nafasi ya Juve ni kubwa zaidi huenda zaidi hata ya maajabu ya soka.

MISIMAMO
LIGI:
                              P         Pts
1       Juventus       29       70
2       AS Roma      29       56
3       Lazio             29       55
4       Fiorentina      29       49
5       Sampdoria     29       48


NYUMBANI:
1       Juventus         15       41
2       Lazio              14       30
3       AS Roma       15       30
4       Sampdoria      14       28
5       Napoli             14       26

 UGENINI:

1       Juventus       14       29
2       AS Roma      14       26
3       Lazio             15       25
4       Fiorentina      15       25
5       Torino           15       21

 MECHI SITA ZA MWISHO:

 Februari 20:
Juventus       2-1       Atalanta     
Machi 2:     
AS Roma       1-1       Juventus     

Machi 9:
Juventus       1-0       Sassuolo     

Machi 14:
Palermo       0-1       Juventus     

Machi 22:
Juventus       1-0       Genoa     

Aprili 2:     
Juventus       2-0       Empoli


TAKWIMU:

                            NYUMBANI       UGENINI     

 Ushindi          13….87%                8….       57%

Sare                 2 ….13%                5….       36%     

 Poteza            0  …. 0%                1….       7%     

JUMLA           15                           14


Fin.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic