April 11, 2015


Nyota wa zamani wa soka wa klabu ya Barcelona ya Hispania, leo Jumamosi wanacheza mechi ya kirafiki na wanasoka wa zamani wa Tanzania kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Baadhi ya nyota hao; Patrick Kluivert, Gaizka Mendieta , Anderson De Soursa ‘Deco’, Francesco Coco na Luis Garcia, waliwasili jana Ijumaa jijini Dar es Salaam kutoka Zanzibar.


Baadhi ya wachezaji hao jana walikuwa Zanzibar kwa mwaliko maalum wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein. Hao ni Simao Sambrosa, Mendieta, Garcia, Luis Enrique, Kluivert na Johan Cruyff.

Kocha wa timu hiyo, Cruyff alisema kuwa wamekuja kuonyesha vipaji vyao vya zamani na hakuna wa kuwazuia kushinda katika mechi ya leo.

“Tupo vizuri, tumejiandaa kwa ajili ya kuweka historia, tunajua wenyeji wataleta upinzani, lakini sisi ndiyo tutakuwa washindi,” alisema Cruyff.

Mratibu wa mechi hiyo kutoka Kampuni ya Primetime Promotions, Stuart Kambona, alisema maandalizi yamekamilika na kikosi cha Tanzania kitakuwa na nyota wa zamani kama Peter Manyika, Juma Kaseja, Shadrack Nsajigwa, Abubakari Kombo, Mustapha Hozza, Salvatory Edward, Dua Said na Yusuph Macho.

Wengine kwa mujibu wa Kambona ni Shaban Ramadhan, Dua Saidi, Nassoro Bwanga, Mohamed Hussein, Steven Nyenge, Mwanamtwa Kihwelu, Edibily Lunyamila, Henry Morris, Haruna Moshi, Bitta John, Madaraka Selemani, Deo Lucas, Bakari Malima, Thomas Kipese, Khatibu Sinapo na Nico Nyagawa.


Kambona alitaja viingilio katika mchezo huo kuwa ni Sh 7,000 kwa viti vya kijani, Sh10,000 (Bluu), Sh 20,000 (Machungwa), Sh30,000 (VIP C), Sh 50,000 (VIP B) na Sh 300,000  kwa VIP A.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic