May 23, 2015


Wakati Yanga ikipiga hesabu za kusajili baadhi ya wachezaji kutoka timu za Ligi Kuu Bara kuimarisha kikosi chake, winga wa zamani wa timu hiyo, Edibily Lunyamila amesema haina haja kwa klabu hiyo kusajili wachezaji wa ndani.


Badala yake Lunyamila akasisitiza, Yanga inapaswa kusajili wachezaji au mchezaji wa kigeni mzoefu ili ifanye vizuri katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao.

“Najua Yanga itakuwa inataka kujaza wachezaji wa kigeni ili kupunguza waliopo pia kuongeza nyota wengine wa ligi ya nchini ili kukiongezea nguvu kikosi.

“Kuhusu hao wa kimataifa sawa hakuna tatizo lakini ukiniambia kuhusu hapa nchini wala siafiki na sijaona sababu ya Yanga kusajili mchezaji wa hapa nchini kwani wana kikosi kinachofanya vizuri. Isajili mchezaji mgeni atakayecheza nafasi ya Ngassa,” alisema Lunyamila.

Wageni walio katika hatari ya kusitishiwa mikataba yao ni Andrey Coutinho raia wa Brazil na Kpah Sherman wa Liberia ambaye ameripotiwa kuhitajika na timu kadhaa nje ya nchi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic