May 23, 2015

SHERMAN.
Straika wa Yanga, Kpah Sherman, ameweka unafiki pembeni na kusema nyota wa Simba, Emmanuel Okwi, kwa jinsi anavyocheza uwanjani, ana uhakika wa kucheza soka popote pale hata nje ya Afrika.

Sherman, raia wa Liberia ambaye alitua Yanga Desemba mwaka jana akitokea Klabu ya Cetinkaya ya Cyprus, amewahi kucheza timu moja na kiungo wa Mtibwa Sugar, Henry Joseph katika kikosi cha Kongsvinger ya Norway.
 
OKWI
Sherman amesema Okwi anajua majukumu yake uwanjani na kwa uwezo wake, anaweza kucheza soka la kulipwa popote pale Afrika hata nje ya bara hili.

“Okwi ni rafiki yangu wa karibu, anacheza kwa kujituma sana, anamiliki mpira, anatumia akili nyingi sana uwanjani na vitu vingine vingi, ambavyo naweza kusema anaweza kucheza popote,” alisema Sherman ambaye ameifungia Yanga mabao sita tangu alipojiunga nayo.

Wakati huohuo, Sherman alisema pengo la winga Mrisho Ngassa aliyejiunga na Free State kwa dau la dola 150,000 (Sh milioni 300) katika timu yao, linahitaji mtu makini kuliziba, vinginevyo timu haitakuwa imara.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic