September 16, 2013


 
AKIWA NA RAIS WA MADRID, PEREZ
Cristiano Ronaldo anaendelea kuwa mfalme wa Real Madrid bila ya kujali kuna ugeni wa Gareth Bale ambaye ni mchezaji ghali zaidi duniani katika uhamisho baada ya pauni milioni 86 kutolewa.


Katika mkataba wake mpya alioingia na Madrid, Ronaldo analipwa karibia mara mbili ya anachopata Bale.


Katika mkataba wake huo mpya anaingiza pauni milioni 15 kwa msimu baada ya kodi lakini kabla ya kupata bonsai yake ya wiki na Bale anaingiza pauni milioni 8.3 kwa msimu.
Wawili hao tayari wameonyesha makali yao katika mechi ya kwanza tu ya La Liga baada ya kila mmoja kufunga bao moja wakati Madrid ilipotoka sare ya mabao 2-2 na Villareal.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic