July 22, 2015


Timu ya African Sports ya Tanga, imeamua kufanya kweli baada ya kupania kumnasa straika wa Yanga, Hussein Javu, kwa nguvu yoyote ile kwa ajili ya kuwasaidia kwenye msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Benchi la ufundi la timu hiyo linaloongozwa na Kocha Mkuu, Mrage Kabange, liameamua kumpitisha Javu baada ya mchujo wa listi ndefu ya mastraika waliyokuwa nayo mkononi.

Lakini imefafanuliwa kuwa awali waliingia hofu ya kupeleka maombi yao hayo Yanga baada ya kusikia fununu za Javu kuhitajika na Majimaji ya Songea na pia mipango ya kupelekwa kwa mkopo Stand United.

Mtu wa ndani wa Sports amelijuza gazeti hili: “Kwa sasa hapa anatafutwa straika na kiungo wa kati, kwenye straika karata imedondoka kwa Javu, kocha ameuagiza uongozi ufanye juu chini kuhakikisha unamnasa kwa kuwa anaamini ni mshambuliaji atakayechangia mafanikio msimu ujao, kwa hiyo harakati zimeshaanza.”


Alipotafutwa Kabange kuizungumzia ishu hiyo, alisema: “Ninachoweza kusema ni kwamba usajili bado unaendelea na bado tupo mawindoni tunaangalia nafasi za wachezaji tunaowataka na wengine tunazungumza nao na kama kutakuwa na chochote basi muda ukifika tutaweka wazi,” alisema Kabange.  

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic