July 21, 2015


Nianze na ule msemo, Milima haikutani….. Hakika ni sahihi baada ya kukutana tena na mshikaji wangu Clever Kazungu.


Huyu jamaa ni mmoja wa waandishi wakongwe na wanaojua vizuri masuala ya soka katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
 

Anatokea Rwanda, lakini anajua mambo mengi sana pia kuhusiana na mpira wa Tanzania hasa ukimueleza kuanzia miaka ya 1970, 1980 anaweza kukupa stori nyingi ambazo hata wewe ulishazisahau.
Yeye ni kati ya waandishi magwiji wa Rwanda, hapa nyumbani wakati fulani aliwahi kufanya kazi ya uchambuzi wa soka katika Gazeti la Championi.

Hatujakutana kwa zaidi ya miaka sita sasa hapa Dar es Salaam, ingawa mara ya mwisho nilikutana naye Kigali, pale Yanga ilipofunga safari kwenda Ikulu ya Rais Paul Kagame.
 
Karibu sana Kazungu, najua uko kwa ajili ya michuano ya Kagame. Lakini Tanzania kwako ni nyumbani, pia nilisikia faraja tumekutana tena.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic