July 20, 2015


Waitaliano wameitumia katuni ya wachezaji wanne wa England wakiwa kwa mganga wa kienyeji.


Mganga huyo anaonekana ni Andrea Pirlo, mkongwe anayekipoga Juventus na timu yao ya taifa ya Azzuri.

Pirlo anaonekana akiwa tiba Raheem Sterling, Theo Walcott, Jordan Henderson na Danny Welbeck.

Lengo la Waitaliano ni kuonyesha Pirlo akiwapa tiba vijana hao waisaidie England. Lakini Waingereza wameona ni kama kubezwa.
 
Nao wakatupia picha mtandaoni Sterling akiwa amemlaba chenga Pirlo hadi akaanguka.

Sasa wanahoji: “Mganga wa aina gani anayetibiwa na mgojwa wake?”
Basi raha tu, kweli mpira haushi vituko na sasa mashabiki hao wanaendelea kulumbana kwenye mitandao ya kijamii hasa Twitter na Instagram.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic