July 20, 2015

 Mshambuliaji mpya wa Manchester City, Raheem Sterling amesema kuondoka kwake Liverpool hakukuwa na nia ya kuwaumiza mashabiki wa klabu hiyo.


Sterrling amejiunga na Man City akitokea Liverpool kwa dau kubwa zaidi la pauni milioni 49 ambalo ni rekodi ya juu ya usajili kwa Waingereza.

Mashabiki wa Liverpool wamekuwa wakimzomea Sterling kila wanapomuona, jambo lililoonyesha kumuumiza.

“Najuta, najisikia vibaya maana halikuwa lengo langu kuwakasirisha,” alisema Sterling.

Ilifikia Sterling alikataa kuongeza mkataba Liverpool baada ya kuwa wamempa mkataba mpya wenye mshahara wa pauni 100,000 kwa wiki.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic