August 5, 2015

 Bondia asiyepigika, Floyd Mayweather amemtosa Mwingereza, Amir Khan na sasa atapigana na bingwa mwingine.


Hilo litakuwa ni pambano la 49 la Mayweather ambaye hajapigwa hata mara moja na linatarajia kufanyika Septemba 12 jijini Las Vegas, Marekani.

Mmarekani huyo anatarajia kuzichapa na Andre Berto ambaye pia ni bingwa wa uzito huo.
 
Pambano lake la mwisho lilikuwa ni dhidi ya Manny Paqcuiao na ushindi wake ulizua mjadala mkubwa mara tu baada ya pambano kwenye ukumbi wa MGM Grand Garden Arena.

Mayweather anakaribia mapambano 50 bila ya kushindwa na yeye amekuwa akisema kwamba pambano lijalo ndilo la mwisho ingawa watu wake wa karibu wanasema atacheza hadi mapambano 50.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic