August 19, 2015


Akipewa mkataba wa miaka mitatu na Yanga, beki mpya wa Yanga, Vincent Bossou, amekumbwa na balaa la kuondolewa katika kikosi cha timu hiyo kitachocheza katika michezo ya Ligi Kuu Bara na kupelekwa katika michezo ya kimataifa.

Bossou ambaye ni raia wa Togo, ni miongoni mwa wachezaji wa kimataifa waliosajiliwa hivi karibuni katika timu hiyo akiwa sambamba na Thabani Kamusoko ‘Ras’ aliyesajiliwa akitokea timu ya FC Platinum ya Zimbabwe.

Yanga inatarajiwa kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao, ikiiwakilisha Tanzania huku Azam ikishiriki Kombe la Shirikisho Afrika.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro, alisema kuwa lengo kubwa la kusajiliwa kwa beki huyo ni kuja kuisaidia timu hiyo katika michezo ya kimataifa ambapo timu hiyo imekuwa ikifanya vibaya.

“Tumeamua kumsajili Bossou baada ya viongozi na benchi la ufundi kuridhishwa na uwezo wake ambao ameuonyesha kwa siku chache ambazo alikuwa katika kikosi chetu katika kambi yetu ya Mbeya.


“Kocha wetu, Mdachi Hans van Pluijm, amepanga kumtumia mchezaji huyu katika michezo ya kimataifa kutokana na uzoefu wake katika michezo hii, hasa kutokana na rekodi yake,” alisema Muro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic