Kiungo mpya wa Yanga, Said Dilunga alijikuta akishindwa kuhimili
kuivaa jezi namba 25 ya beki wa pembeni wa Simba, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’
kwenye mechi ya Nani Mtani Jembe uliozikutanisha timu hizo na kujikuta akiitoa
na kuvaa fulana ya mazoezi.
KIIZA AKIMPA NENO DILUNGA KUHUSIANA NA JEZI NAMBA 25 |
Tukio hilo lilitokea mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo ulioisha
kwa Simba kushinda mabao 3-1 ambapo kiungo huyo alibadilishana jezi ya juu na
beki huyo mwenye umbo dogo na kasi awapo uwanjani.
DILUNGA ANAONEKANA KUELEWA SOMO HUKU KIIZA AKIWA SIRIAZ KINOMA KAMA AFANDE |
SOMO LIMEELEWEKA, ANAIVUA JEZI HIYO YA ZAMANI YA OKWI |
SALEHJEMBE ililishuhudia tukio hilo mwanzo mwisho
lilimuona kiungo huyo baada ya kubadilishana akaitwa na mshambuliaji wa Yanga,
Hamis Kiiza na kunong’onezana kitu, walipomaliza Dilunga akaitoa jezi hiyo
iliyokuwa ikivaliwa na Emmanuel Okwi kipindi yupo Simba ambaye kwa sasa yupo
Yanga kisha akaichukua ya Yanga na kuivaa.
Alipotafutwa Dilunga ili kujua sababu za kuitoa jezi hiyo huku
wachezaji wenzake wa Yanga wakiwa na uzi wa watani zao hao alisema “Jezi ile
niliamua tu kuitoa na kuvaa ya mazoezi lakini niliondoka nayo na nipo nayo hapa
nyumbani. Baba Ubaya ni rafiki yangu na nimewahi kucheza naye kipindi cha
nyuma.”
0 COMMENTS:
Post a Comment