August 22, 2015


Mshambuliaji Papa Niang amepewa Jumatatu kama nafasi ya kuwadhihirishia Simba kwamba ana uwezo na atakuwa msaada, hivyo chaguo lake, ashindwe arudi Senegal, afanye vitu apande meli ya Simba.


Niang raia wa Senegal ambaye amewasili nchini jana na kujiunga na Simba, anasubiri siku hiyo ambayo Simba itacheza na MWadui FC kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kumshawishi kocha Dylan Kerr na benchi zima la ufundi kwamba anaweza.

Lakini Niang ataitumia nafasi hiyo pia kuwashawishi viongozi wa Simba kwamba wanastahili kumwaga mamilioni ili kupata saini yake.

Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema kila kitu kuhusiana na mechi hiyo kimekamilika.


“Ni kweli mwalimu atamtumia Papa Niang ikiwa ni sehemu ya majaribio yake mafupi na kupata uhakika kuwa ni mshambuliaji wa kiwango tunachotaka.

“Pia tunaamini ni nafasi ya mashabiki wa Simba kumuona mchezaji huyo na kikosi chao kwa ujumla na wanaweza pia wakawa na mchango wao,” alisema Kaburu.

Kuhusiana na mechi kuchezwa Jumatatu, Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Simba, Haji Manara amesema inawezekana ikawa tofauti lakini ndiyo mabadiliko ya kisoka duniani.

“Unajua England sasa wana mechi zinazochezwa Jumatatu, hizo ni mechi za Ligi Kuu England. Hapa pia tutaenda tunabadilika taratibu na itawezekana.

“Tunaamini kunaweza kuwa na usumbufu kidogo, lakini tutaenda tunazoea. Ninachowashawishi mashabiki wa Simba, wapenda mpira wote wafike uwanjani.

“Pia kutakuwa na nafasi ya kumuona mshambuliaji Papa Niang akiichezea Simba, pia kupata uhakika kutokana ana uwezo wake,” alisema Manara.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic