October 22, 2015


Azam FC imeendeleza vipigo baada ya kushinda mechi yake ya sita huku ikiwa na sare moja.


Ikiwa ugenini, Azam FC imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya wenyeji wake Ndanda FC katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Nangwanda mjini Mtwara.

Azam FC imepata ushindi kwa bao pekee lililofungwa na beki wake wa kulia, Shomari Kapombe.
Pamoja na mechi kuwa nzuri, hali ya uwanja ilionekana kuwapa wakati mgumu wachezaji wa Azam FC.


Kutokana na ushindi huo, Azam FC imefikisha pointi 19 sawa na Yanga ambayo iko kileleni na Azam Fc inabaki katika nafasi ya pili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic