October 21, 2015


Timu ya Yanga leo inashuka uwanjani kupambana na Toto Africans ya Mwanza, katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, Yanga itawakosa baadhi ya nyota wake wa kutumainiwa walioumia wikiendi iliyopita ilipopambana na Azam FC kwenye uwanja huo.

Kutokana na hali hiyo kocha mkuu wa timu hiyo, Mholanzi, Hans van Der Pluijm, atalazimika kukipanga upya kikosi chake tayari kwa kukabiliana na Toto Africans ambayo inafundishwa na Mjerumani, Martine Grelics.

Nyota wa Yanga watakaoikosa mechi hiyo ni Mbuyu Twite ambaye alipasuka juu ya jicho na kushonwa nyuzi tano baada ya kugongwa na mchezaji wa Azam pamoja na Salum Telela ambaye anasumbuliwa na maumivu ya kifundo cha mguu.

Akizungumza na Championi Jumatano, Pluijm alisema kuwa kutokana na hali hiyo, hatawatumia wachezaji hao katika mechi hiyo ya leo na badala yake nafasi zao zitachukuliwa na wengine ambao wapo fiti.

“Nitawakosa Twite na Telela katika mechi hiyo kutokana na kuwa majeruhi lakini nitawatumia waliopo kuhakikisha tunaibuka na ushindi katika mechi hiyo.”
Wachezaji wanaotarajiwa kuziba nafasi hizo ni Deus Kaseke atakayechukua nafasi ya Twite na Haruna Niyonzima atakayechukua nafasi ya Telela.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic