Kiungo wa pembeni wa Royal Eagles ya
Afrika Kusini, Uhuru Selemani, thamani yake imefikia Sh milioni 125 iwapo suala
la kumuuza litafikia.
Mtandao wa transfer market umempa uhuru
thamani hiyo kwa kusema anaweza kuuzwa euro 50,000.
Mtanzania huyo amechukua nafasi ya pili
katika wachezaji watatu wa kulipwa walio katika kikosi hicho kinachoshiriki
daraja la kwanza nchini humo.
Kiungo Mnigeria, Prince Olomu amepewa
thamani ya euro 250,000 ambaye ndiye ghali zaidi ya wachezaji wote wa kikosi
hicho.
Mgeni anayeshika nafasi ya tatu kwa
thamani ya manunuzi katika kikosi hicho ni kipa kutoka Ivory Coast, Noel Yobou
ambaye amepewa euro 25,000 ikiwa ni nusu ya thamani ya Uhuru.
Uhuru anaichezea timu hiyo ya jijini
Darbun kwa mkopo akitokea Jomo Cosmos.
Keep It Up..... Uhuru Selemani. Hapo Bongo kipaji chako kilikuwa kinafujwa tu.
ReplyDelete