Na
Saleh Ally
KUMEKUWA
na lawama chungu mzima kuhusiana na suala la vyombo vya habari kulalia katika
mchezo wa soka huku michezo mingine ikisahaulika.
Lawama
hizo zinasukumwa kwa wanahabari, mmoja wao mimi kwamba tumejisahau kupindukia
na tunachoona kinafanya vema ni soka pekee.
Sijawahi
kukataa kwa asilimia mia kwamba kweli hapo kuna tatizo kidogo kwa upande wa
wanahabari kujisahau na huenda malezi ya uandishi, hasa kwa sisi ambao tunapata
nafasi ya kufunza wengine, lazima tusisitize kuendelea kuijali michezo mingine.
Wakati
sisi tunajitahidi kuwafundisha waandishi wengine, kuwakumbusha pia wengine,
basi huenda uwe wakati wa wahusika wa michezo mingine nao kuamka na kuacha
mambo mengi wanayoendelea nayo katika kipindi hiki.
Ningependa
nitumie zaidi mfano wa mchezo wa riadha ambao katika miaka ya 1970, 1980 na
mwanzoni mwa 1990 ulijenga heshima kubwa kwa taifa letu kupitia wanariadha
mbalimbali kama Juma Ikangaa, Filbert Bayi na wengineo.
Majina
yao sasa ni makubwa katika nchi nyingi, mfano Juma Ikangaa, nimeelezwa hadi
wamefikia kuupa mtaa jina lake kutokana na heshima.
Ikangaa
ameshinda au kufanya mashindano kibao kama New York Marathon, Boston Marathon,
Tokyo Marathon na mengineyo na alifanya hivyo kwa uwezo wake na nidhamu ya juu
kabisa.
Lakini
niwaulize watu wa riadha, kabla ya kuanza kulaumu wanahabari, sasa wanamtumiaje
mtu kama Ikangaa ambaye huenda Japan au Marekani wangependa kuwa naye kwa ajili
ya kuwaendeleza tu vijana wao.
Niwaulize
tena, wamewahi kumuenzi vipi mtu kama Ikangaa? Serikali, imemsahau, watu wa
riadha wamemsahau na sasa badala ya riadha, migogoro ni kibao, kila kukicha ni
majungu.
Sasa
mnataka kuripotiwa nini zaidi ya migogoro na utumbo ambao hauna lengo la
kuendeleza michezo na badala yake malumbano na watu kutaka kushibisha matumbo
yao?
Kina
Ikangaa na Bayi wapo, hawatumiki lakini angalia mtu kama Selemani Nyambui,
ameondoka nchini kwa mara nyingine na safari hii amekwenda kufundisha Brunei.
Wakati
akiwa hapa, karibu alipokuwa akisikika basi ilikuwa ni malumbano tu kwa kuwa ni
kiongozi wa chama cha riadha. Leo anaendeleza au kukuza vijana wa nchi nyingine
ambazo zinajua umuhimu wa kuwakuza na kuwaendeleza vijana.
Ikangaa
hata angekuwa mshauri bado ingekuwa ni jambo zuri kwa riadha nchini kwa kuwa
pamoja na ubora wa kazi yake akiwa mwanariadha lakini ni askari wa jeshi
mstaafu.
Wote
tunajua nidhamu ya jeshi, Ikangaa amefikia moja ya vyeo vya juu na hiyo ni
sehemu ya kuonyesha kiasi gani alikubalika na kupewa heshima kicheo. Cheo
kinapatikana kwa heshima kiutendaji.
Utendaji
wake lazima ulikuwa bora, ndiyo maana hadi anastaafu aliendelea kuwa mmoja wa
askari waliokubalika. Achana na hivyo, Ikangaa kielimu pia ana elimu nzuri, ni
mtu aliyekwenda shule.
Angalia
hapa, kipaji chake, nidhamu, elimu nzuri lakini bado watu wa riadha hawaoni
kama wanaweza kumtumia kuusaidia mchezo wa riadha na badala yake
kinachoangaliwa ni hofu kwamba akiwa karibu huenda atakuwa mkali na wengine
watashindwa kupata nafasi ya ‘kupiga’ na kujifaidisha.
Watanzania
tuna tabia ya kuwahofia watu wenye nidhamu katika kazi au watu wanaopeleka
mambo katika mpangilio unaotakiwa.
Tanzania
tunawahofia watu ambao ni wachapakazi kwa kuwa tunajua watatuumbua na kuonyesha
rundo la upungufu tunaokuwa nao.
Ikangaa
mkimpa matofali kujenga ukuta bora wa riadha, kamwe hamhitaji hata kumueleza
mnataka nini. Huenda yeye ndiye atawafundisha zaidi nini cha kufanya.
Huu
ndiyo wakati sasa, acheni kulialia kwamba hamuandikwi, hamtangazwi au kuonekana
kwenye runinga. Pigeni moyo konde mbadili gia angani na watu kama Ikangaa, Bayi
na wengine, watumike vizuri kuusaidia mchezo wa riadha ili ukiripotiwa, basi
mafanikio yawepo na si kama sasa, majungu kibaooo.
TAFADHARI NI-FOLLOW(Instagram;
salehjembe. Twitter; salehjembe)
0 COMMENTS:
Post a Comment